Methali za Kiswahili

Searching for Methali za Kiswahili. Today we are going to look at Methali za Kiswahili. You can use them in your saying or writing Isha.

A

  • Ada ya mja hunena, mwungwana ni kitendo.
  • Adhabu ya kaburi aijua maiti
  • Afua ni mbili, kufa na kupona.
  • Ahadi ni deni.
  • Aibu ya maiti, aijua mwosha.
  • Ajali haina kinga wala kufara
  • Aisifuye mvua, imemnyeshea.
  • Akiba haiozi.
  • Ajidhaniye amesimama, aangalie asianguke.
  • Asifuye mvuwa imemnyea.
  • Akili nyingi huondowa maarifa.
  • Akili ni nywele; kila mtu ana zake.
  • Akitaka kaa, mpe moto.

Read: Kiswahili Insha Examples

  • Akipenda chongo huita, huona kengeza.
  • Akufukuzaye hakwambii, Toka.
  • Akupaye kisogo si mwenzio.
  • Akumulikaye mchana; usiku akuchoma.
  • Aliyekando, haangukiwi na mti.
  • Alalaye usimwamshe; ukimwamsha, utalala wewe.
  • Aliyeko juu, mungojee chini.
  • Amani haipatikani ila kwa ncha ya upanga.
  • Amnyimae punda adesi, kampunguzia mashuzi.
  • Asiye kuwapo na lake halipo.
  • Asiyefunzwa na mamaye, hufunzwa na ulimwengu
  • Asiyekuwapo na lake halipo.
  • Asiyekujua hakuthamini.
  • Asiye kubali kushindwa si mshindani.
  • Asiyesikia la mkuu, huvunja guu
  • Atangaye na jua hujuwa.
  • Avumaye baharini papa kumbe wengi wapo.
  • Avuaye nguo huchutama.

B

  • Baada ya kisa mkasa. Baada ya chanzo kitendo.
  • Baniani mbaya kiatu chake dawa.
  • Baada ya dhiki faraja.
  • Bendera hufuata upepo.
  • Baniani mbaya kiatu chake dawa.
  • Bora afya kuliko mali.
  • Bilisi wa mtu ni mtu.

Read: KCPE Kiswahili Revision Paper With Answers

C

  • Chanda chema huvikwa pete.
  • Chamlevi huliwa na mgema.
  • Cha kuvunda, hakina ubani.
  • Chema chajiuza, kibaya chajitembeza
  • Chombo cha kuzama hakina usukani.
  • Chembe na chembe ni mkate.
  • Cha kichwa kitamu, na cha mkia kitamu.
  • Chovya chovya yamaliza buyu la asali.
  • Cha kuvunja, hakina rubani.
  • Chema hakikai
  • Chombo kilichopikiwa samaki hakiachi kunuka vumba.
  • Chui hageuki madoamadoa
  • Chungu kikuu, hakikosi ukoko.

Read: African Proverbs

D

  • Dalili ya mvua mawingu.
  • Dau la mnyonge haliendi joshi; likienda joshi ni mungu kupenda.
  • Damu nzito kuliko maji.
  • Debe shinda haliachi kutika.
  • Dawa ya moto ni moto.
  • Dunia duwara.
  • Dua la kuku halimpati mwewe.
  • Duniani ni msiba na furaha, kuna ugonjwa na siha.
  • Dunia huleta jema na ovu.
  • E
  • Elimu bahari, haina kuta wala dari.
  • F
  • Fadhila ya punda ni mateke.
  • Faragha ya nyani, huishia ngokoni
  • Fimbo ya mbali hayiuwi nyoka.
  • Fahali wawili hawakai zizi moja.
  • Fuata nyuki ule asali.
  • Fedha fedheha.
  • Fumbo mfumbe mjinga mwerevu huligangua.
  • Fungato haliumizi kuni.

Read: Debate Motions for Secondary Schools in Kenya

G

  • Ganda la mua la jana chungu kaona kivuno.

H

  • Haba na haba hujaza kibaba.
  • Habari ya uwongo, ncha zake saba, habari ya kweli, ncha yake moja.
  • Hapana marefu yasio na mwisho.
  • Hakuna bahari, isiyo na mawimbi.
  • Hakuna siri ya watu wawili.
  • Haraka haraka haina baraka.
  • Hasira, hasara.
  • Hasira za mkizi, tijara ya mvuvi
  • Hakuna kisicho badali.
  • Heri kufa macho kuliko kufa moyo.
  • Heri kujikwa kidole kuliko ulimi.
  • Hiari ya shinda utumwa.
  • Hucheka kovu asiye kuwa na jeraha.
  • Hapana marefu yasio na mwisho.
  • Heri kuliwa na simba, kuliko kuliwa na fisi.
  • Hucheka kovu asiye kuwa na jeraha.

J

  • Jina jema hungara gizani.
  • Jitihadi haiondoi kudura ya mungu.
  • Jogoo la shamba haliwiki mjini.
  • Jino la pembe si dawa ya pengo.
  • Jivu halijai, gao la mkono.

Read: CBC Curriculum Structure

K

  • Kamba hukatika pabovu.
  • Kafiri akufaye si Isilamu asiyekufa.
  • Kama chanda na pete.
  • Kanga hazai ugenini.
  • Kata pua uunge wajihi
  • Kawia ufike
  • Kazi mbaya siyo mchezo mwema.
  • Kelele za mlango haziniwasi usingizi.
  • Kenda karibu na kumi.
  • Kidole kimoja hakivunji chawa.
  • Kidogo ni tamu, kingi ni sumu.
  • Kichache hakikutoshi na kingi hakikulishi.
  • Kiburi si maungwana.
  • Kikulacho ki nguoni mwako.
  • Kila mlango na ufunguo wake.
  • Kila chombo kwa wimbile.
  • Kingiacho mjini si haramu.
  • Kila ndege huruka na mbawa zake.
  • Kimya kingi kina mshindo mkubwa.
  • Kinyozi hajinyoi, akinyoa kujikata.
  • Kipendacho moyo ni dawa.
  • Kipofu haonyi njia.
  • Kila mwamba ngoma ,ngozi huivuta kwake.
  • Kila ndege mwenye mkia ni lazima aringe.
  • Kilio huanza mfiwa ndipo wa mbali wakaingia.
  • Kinga na kinga ndipo moto uwakapo.
  • Kinolewacho, hukata.
  • Kilichomo baharini, kakingojee ufukoni.
  • Kiozacho hutoa uvundo
  • Kipofu hasahau fimbo yake
  • Kinywa ni jumba la maneno.
  • Kipya kinyemi ingawa kidonda.
  • Kisokula mlimwengu,sera nale.
  • Kitanda usicho kilala hujui kunguni wake.
  • Kivuli cha fimbo hakimfichi mtu jua.
  • Kizuri chajiuza kibaya chajitembeza.
  • Kiwi cha yule ni chema cha;hata ulimwengu uwishe.
  • Kobe atakufa asipojikuna nyumaye mwenyewe.
  • Kosa moja haliachi mke.
  • Konzo ya maji haifumbatiki
  • Kozi mwandada, kulala na njaa kupenda.
  • Kufa kikondoo, ndiko kufa kiungwana.
  • Kufa kufaana.
  • Kuchamba kwingi,kuondoka na mavi.
  • Kuku havunji yai lake.
  • Kukopa harusi, kulipa matanga.
  • Kufa kwa mdomo, mate hutawanyika.

Read: 100 Positive Behavior Quotes for Students

  • Kuku mgeni hakosi kamba mguuni.
  • Kuku wa maskini hatagi mayai.
  • Kuku mwenye watoto, halengwi jiwe.
  • Kucha M’ngu si kilemba cheupe.
  • Kufa si suna,ni faradhi.
  • Kujikwa si kuanguka, bali ni kwenda mbele.
  • Kulea mimba si kazi, kazi kulea mwana.
  • Kuagiza kufyekeza.
  • Kunguru mwoga hukimbiza mbawa zake.
  • Kunako matanga kumekufa mtu.
  • Kumpa mwenzio si kutupa, ni akiba ya mbeleni.
  • Kupanda mchongoma ,kushuka ngoma.own.
  • Kupotea njia ndiyo kujua njia.
  • Kutoa ni moyo usambe ni utajiri.
  • Kusikia si kuona.
  • Kuuliza si ujinga.
  • Kutu kuu ni la mgeni.
  • Kwenye miti hakuna wajenzi.
  • Kwenda mbio siyo kufika.
  • Kweli iliyo uchungu si uwongo ulio mtamu.

L

  • La kuvunda (kuvunja)halina ubani.
  • Lake mtu halimtapishi bali humchefusha.
  • La kuvunda halina rubani.
  • Leo ni leo asemayo kesho ni mwongo.
  • Lisemwalo lipo,ikiwa halipo laja.
  • Leo uko, kesho huko.
  • Liandikwalo ndiyo liwalo.
  • Likitoka liote.
  • Lipitalo ,hupishwa .
  • Lifaalo kueleza lieleze, lisilofaa limeze.
  • Lila na fila hazitangamani.
  • Lisilokuwapo moyoni, halipo machoni.
  • Lisilo na mkoma, hujikoma lilo.

Read: Best Quotes about Education

M

    • Macho hayana pazia.
    • Maafuu hapatilizwi.
    • Mafahali wawili hawakai zizi moja.
    • Maisha hayana pato, hutupita kama ndoto.
    • Mahaba haiwi mlango.
    • Maiti haulizwi sanda.
    • Maji ukiyavuliya nguo huna budi kuyaogelea.
    • Maji hufuata mkondo.
    • Maji huteremka bondeni, hayapandi mlima.
    • Maji yakija hupwa.
    • Maji usiyoyafika hujui wingi wake.
    • Maji yakimwagika hayazoleki
    • Maji ya nazi, yataka uvugulio tu.
    • Maji yakija hupwa.
    • Maji yaenda njia yake.
    • Maji ya kifuu ni bahari ya chungu.
    • Maji ya moto, hayachomi nyumba.
    • Majumba makubwa husitiri mambo.
    • Mpanda ngazi hushuka.
    • Majuto ni mjukuu.
    • Mali ya bahili huliwa na wadudu.
    • Mambo ya mbele, giza ya wele
    • Mambo ya nyumba, ni kinga.
    • Manahodha wengi chombo huenda mrama.
    • Maneno mema hutowa nyoka pangoni.
    • Maneno makali hayavunji mfupa.
    • Maneno mengi si haja, maneno mengi si huja.
    • Masikini akipata matako hulia mbwata.
    • Maskini haokoti, akiokota huambiwa kaiba.
    • Maskini na mwanawe, tajiri na mali yake.
    • Masikio hayapiti kichwa.
    • Mapema maivu, mapema maovu.
    • Mapaka wengi, hayamkamati panya.
    • Mapenzi ni kikohozi, hayawezi kufichika.
    • Mapenzi ni majani, popote penye mbolea huotea.
    • Mara changu, mara chako
    • Mavi usioyala,wayawingiani kuku?
    • Mavi ya kale hayanuki.
    • Mbio za sakafuni huishia ukingoni.
    • Mbinu hufuata mwendo.
    • Mbiu ya mgambo ikilia ina jambo.
    • Mbuzi wa maskini, hazai mapacha
    • Mbwa hafi maji, akiona ufuko.
    • Mbinu hufuata mwendo.
    • Mbuge hawezi kujenga nyumba.
    • Mbuzi wa mkata, atakufa utasa.
    • Mchagua jembe si mkulima.
    • Mcheka kilema, hafi bila kumfika.
    • Mchelea mwana kulia hulia yeye.
    • Mchelea bahari si msafiri.
    • Mchagua nazi, hupata koroma.
    • Mchakacho ujao,halulengwi na jiwe.
    • Mchama ago hanyeli, huenda akauya papo.
    • Mchana semani usiku lalani.
    • Mchele moja mapishi mengi.
    • Mcheka kilema hafi bila kumpata.
    • Mcheza kwao hutuzwa.
    • Mchimba kisima huingia mwenyewe.
    • Mcheza na tope humrukia.
    • Mcheza hawi kiwete, ngoma yataka matao.
    • Mchezea zuri, baya humfika.
    • Mchimba kisima, hakatazwi maji.
    • Mchovya asali hachovi mara moja.
    • Mchonga mwiko hukimbiza mkono wake.
    • Mchuma janga hula na wakwao.
    • Mchumia juani,hula kivulini.
    • Mchuma janga hula na wakwao.
    • Mchunga haziki.
    • Mdharau biu hubiuka yeye.
    • Mema na mabaya ndio ulimwengu.
    • Meno ya mbwa hayaumani.
    • Mficha uchi hazai.
    • Mfa maji hukamata maji.
    • Mfinyazi hulia gaeni.
    • Mgaagaa na upwa hali wali mkavu.
    • Mgema akisifiwa tembo hulitia maji.
    • Mganga hajigangui.
    • Mfukuzwa kwao hana pakwenda.
    • Mgeni ni kuku mweupe.
    • Mgonjwa haulizwi uji.
    • Mgeni njoo mwenyeji apone.
    • Mgonjwa haulizwi uji.
    • Miye nyumba ya udongo, sihimili vishindo.
    • Milima ya mbali, haina mawe
    • Mjinga akierevuka mwerevu yupo mashakani.
    • Mjumbe hauawi.
    • Mkamatwa na ngozi ndiye mwizi.
    • Mkeka mpya haulaliwi vema.
    • Mkamia maji hayanywi.
    • Mkono moja haulei mwana.
    • Mkono moja hauchinji ngombe.
    • Mkono mtupu haulambwi.
    • Mkono usioweza kuukata, ubusu.
    • Mkosa jembe halimi
    • Mkono wa kuume, haukati wa kushoto.
    • Mkosa kitoweo humangiria.
    • Mke ni nguo ,mgomba kupalilia.
    • Mkosa titi la mama, hata la mbwa hulamwa.
    • Mkulima ni mmoja walaji ni wengi.
    • Mkuki kwa nguruwe mtamu,kwa mwanadamu uchungu.
    • Mla cha mwenziwe na chake huliwa.
    • Mla kuku wa mwenziwe miguu humwelekeya.
    • Mla nawe hafi nawe ila mzaliwa nawe.
    • Mla mla leo mla jana kala nini?
    • Mla mbuzi hulipa ngombe.
    • Mla cha uchungu na tamu hakosi.
    • Mla kwa miwili, hana mwisho mwema.
    • Mlenga jiwe kundini hajui limpataye.
    • Mlevi wa mvinyo hulevuka, mlevi wa mali halevuki.
    • Mlimbua nchi ni mwananchi.
    • Mlinzi hulinda ndege, mke mzuri halindwi.
    • Mnyonge hana hasira.
    • Moja shika,si kumi nenda urudi.
    • Mmoja hashui chombo.
    • Mnyamaa kadumbu.
    • Mnywa maji kwa mkono moja,Kiu yake i pale pale.
    • Mnyonyore haunuki, hupendeza maua yake.
    • Mnyonge hupata haki, ni mwenye nguvu kupenda.
    • Moto hauzai moto.
    • Moja shika, kumi hutapata
    • Moja shika si kumi nenda urudi.
    • Moto wa kumvi,hudumu.
    • Mpanda ngazi hushuka.
    • Mpanda farasi wawili hupasuka msamba.
    • Mpemba akipata gogo hanyii chini.
    • Mpanda ovyo hula ovyo.
    • Mpemba hakimbii mvua ndogo.
    • Mpende akupendaye.
    • Mpofuka ukongweni,hapotewi na njia
  • Mpiga ngumi ukuta huumiza mkonowe.
  • Msafiri masikini ajapokuwa sultani.
  • Msema kweli, hana wajoli.
  • Mshoni hachagui nguo.
  • Mshale usiyo na nyoya, hauendi mbali.
  • Msasi haogopi mwiba.
  • Mshale kwenda msituni haukupotea.
  • Msema pweke hakosi.
  • Mshika mawili, moja humponyoka.
  • Msitukane wagema na ulevi ungalipo.
  • Msitukane wakunga na uzazi ungalipo.
  • Msika mavi, hayaachi kumnuka.
  • Msi chake ni mwenda zake.
  • Mstahimilivu hula mbivu.
  • Mtaka nyingi nasaba hupata mwingi msiba.
  • Mtaka yote hukosa yote.
  • Mtafunwa na nyoka akiona ung’ongo husitika.
  • Mtaka cha mvunguni sharti ainame.
  • Mtaka unda haneni.
  • Mtegemea nundu haachi kunona.
  • Mtaka yote kwa pupa, hukosa yote.
  • Mtembezi hula miguu yake.
  • Mteuzi hashi tamaa.
  • Mtego bila ya chambo, haunasi.
  • Mtenda mema hasemi, akisema hatendi.
  • Mti hauendi ila kwa nyenzo.
  • Mti huponzwa na tundaze.
  • Mti upigwao mawe ni mti wenye matunda.
  • Mtoto akililia wembe mpe.
  • Mtoto wa nyoka ni nyoka.
  • Mtoto umleyavyo ndivyo akuavyo.
  • Mtondoo haufi maji.
  • Mtoto akibebwa, hutazama kisogo cha mamaye.
  • Mtu hujikuna ajipatiapo.
  • Mtumi wa kunga haambiwi maana.
  • Mtu akimpa maskini kichache, Mungu humruzuku kingi.
  • Mtupa jongoo hutupa na mti wake.
  • Mtu aliyeumwa na nyoka akiona ung’ongo hushtuka.
  • Mtu apandacho (kitu), ndicho avunacho.
  • Mtu pweke, ni uvundo.
  • Mtu asiye na akili, usifuatane naye.
  • Mtu huenda na uchao, haendi na utwao.
  • Mtu hakatai mwito,hukata aitwalo.
  • Mtu halindi bahari, ipitayo kila chombo.
  • Mtu hasafiri nyota ya mwenziwe.
  • Mtu huulizwa amevaani haulizwi amekulani.
  • Mtumi wa kunga haambiwi maana.
  • Mtumikie kafiri upate mradi wako.
  • Mtumai cha ndugu hufa masikini.
  • Mume wa mama ni baba.
  • Mtunza bahari, siye msafiri.
  • Mtumikie kafiri upate mradi wako.
  • Mtulivu hula mbivu.
  • Mtupa jongoo hutupa na mti wake.
  • Mume ni kazi, mke ni nguo.
  • Mungu akikupa kilema, hukupa na mwendo wake.
  • Mume wa mama ni baba.
  • Mungu hapi kwa mvua, wala hanyimi kwa jua.
  • Muhogo mchungu, usiuchezee.
  • Mungu hamfichi mnafiki.
  • Muuliza hujibiwa ili apate fahamu.
  • Mvuvi ajuwa pweza alipo.
  • Mvumbika changa hula mbovu.
  • Mvunja nchi ni mwananchi.
  • Mvungu mkeka.
  • Mvuvi ajuwa pweza alipo.
  • Mwamini Mungu si mtovu.
  • Mwana kila mwaka, ni kubwa baraka.
  • Mwacha asili ni mtumwa.
  • Mwamba na wako hukutuma umwambiye.
  • Mwana maji wa kwale kufa maji mazowea.
  • Mwana mkaidi hafaidi mpaka siku ya Idi.
  • Mwana mkuwa nawe ni mwenzio kama wewe.
  • Mwanadamu atakufa, jina lake litakaa.
  • Mwanamaji, hutaraji kufa maji.
  • Mwanamume ni mbono, hualikia kule.
  • Mwana wa kuku hafunzwi kuchakura.
  • Mwanga mpe mtoto kulea.
  • Mwana simba ni simba.
  • Mwanzo kokochi mwisho nazi.
  • Mwana wa mtu ni kizushi; akizuka, zuka naye.
  • Mwangaza mbili moja humponyoka.
  • Mwanzo wa ngoma ni lele.
  • Mwanzo wa chanzo ni chane mbili.
  • Mwenda bure si mkaa bure huenda akaokota.
  • Mwenda mbio hujikwa kidole.
  • Mwenye kelele hana neno.
  • Mwenye huba, hana dawa, ila kwa muhibiwa.
  • Mwekaji kisasi haambiwi mwerevu.
  • Mwapiza la nje hupata la ndani.
  • Mwekaji kisasi haambiwi mwerevu.
  • Mwenda tezi na omo marejeo ngamani.
  • Mwenye chake, hakosi cha mwenziwe
  • Mwenye nguvu mpishe.
  • Mwenye pupa hadiriki kula tamu.
  • Mwenye kovu, usidhani kapoa.
  • Mwenye kuchinja hachelei kuchuna.
  • Mwenye shibe hamjui mwenye njaa.
  • Mwenye kutafuta, hakosi kupata.
  • Mwenye shoka hakosi kuni.
  • Mwenye kovu, haliwai na kidonda.
  • Mwenye kovu usidhani kapowa.
  • Mwenye kupenda ni juha.
  • Mwenye kuchinja hachelei kuchuna.
  • Mwenye kisu kikali ndiye alaye nyama.
  • Mwenye kupanda ngazi, na mwenye kushuka ngazi, hawapeani mkono.
  • Mwenye macho, haambiwi tazama.
  • Mwenye kuumwa na nyoka akiona jani hushtuka.
  • Mwenye njaa hana miiko.
  • Mwenye shibe hamjui mwenye njaa.
  • Mwenye tumbo ni tumbole, angafunga mkaja.
  • Mwenzako akinyolewa wewe tia maji
  • Mwili wa mwenzio ni kando ya mwilio.
  • Mwibaji na watwana, mlifi ni mwungwana.
  • Mwiba wa kujitoma, hauambiwi pole.
  • Mwizi, siku zake ni arobaini
  • Mwosha hadhuru maiti.
  • Mwosha husitiri maiti.
  • Mwomba chumvi huombea chunguche.
  • Mzazi haachi ujusi.
  • Mzigo wa mwenzio ni kanda la usufi.
  • Mzoea punda, hapandi farasi.
  • Mzowea kutwaa, kutoa ni vita.
  • Mzika pembe ndiye mzua pembe.
  • Mzoea udalali, duka haliwezi.
  • Mzungu Wa kula hafundishwi mwana.

N

  • Nahodha wengi, chombo huenda mrama.
  • Nazi mbovu harabu ya nzima.
  • Ndege mjanja hunaswa na tundu bovu
  • Ncha na ncha, hazichomani
  • Ndugu mwui afadhali kuwa naye.
  • Ndugu chungu, jirani mkungu.
  • Ndege mwigo hana mazowea.
  • Na tuone ndipo twambie, kusikia si kuona.
  • Ndege hulindwa, mke halindwi.
  • Ndimi arobaini, mafundo arobaini.
  • Ndugu wakigombana, chukua jembe ukalime, wakipatana chukua kikapu ukavune.
  • Ndovu halemewi na pembe zake.
  • Neno ulikataalo, ndilo Mungu apendalo.
  • Ngoja! ngoja? huumiza matumbo.
  • Ngoma ivumayo haidumu.
  • Ngozi ivute ili maji.
  • Ng’ombe haelemewi na nunduye.
  • Ng’ombe avunjikapo guu hurejea zizini.
  • Ngoma ivumayo haikawii kupasuka.
  • Nguruwe aendealo, ndilo atendalo.
  • Nguo za kuazima, hazisitiri matako.
  • Nifae na mvua nikufae na jua.
  • Ni heri mbichi, kama ya kwoka.
  • Ni jambo lipi, lisilo na nduguye, na mwamu wake.
  • Nia njema ni tabibu, nia mbaya huharibu.
  • Nimekula asali udogoni, utamu ungali gegoni.
  • Njia ya mwongo fupi.
  • Njaa ya leo, ni shibe ya kesho.
  • Njema haziozi.
  • Njia ya siku zote haina alama.
  • Nyota haionekani mchana.
  • Nyani haoni kundule, huliona la mwenziwe.
  • Nta si asali nalikuwa nazo si uchunga.
  • Nyoka, mlinzi wa pango lake.
  • Nyumba haikimbii.
  • Nyumba usiyolala ndani huijui ila yake.
  • Nzi kufa juu ya kidonda Si haramu.
  • Nyumba ya udongo haihimili vishindo.
  • Njia mbili zilimshinda mzee fisi, alipasuka msamba.

P

  • Padogo pako Si pakubwa pa mwenzako.
  • Paka akiondoka, panya hutawala.
  • Pabaya pako si pema pa mwenzako.
  • Painamapo ndipo painukapo.
  • Paka wa nyumba haingwa.
  • Paka hakubali kulala chali.
  • Papo kwa papo kamba hukata jiwe.
  • Panapo wengi hapaharibiki neno.
  • Pema usijapo pema; ukipema Si pema tena.
  • Penye kuku wengi hapamwagwi mtama.
  • Penye mafundi, hapakosi wanafunzi.
  • Penye dhiki, hakuna chuki.
  • Penye miti hakuna wajenzi.
  • Penye urembo ndipo penye urimbo.
  • Penye nia ipo njia.
  • Penye wazee haliharibiki neno.
  • Penye wengi pana mengi.
  • Penye wengi pana Mungu.
  • Pesa na zawadi hufanya miadi.
  • Pilipili usozila zakuwashiani?
  • Pwagu hupata pwaguzi.
  • Punda haendi ila kwa kigongo.
  • Punge moja ya mtama, ni bora kuliko almasi.
  • Pofu hasahau mkongoja wake.

R

  • Radhi ni bora kuliko mali

S

  • Samaki mmoja akioza, huoza wote.
  • Sahani iliyofunikwa, kilichomo kimesitirika.
  • Shimo Ia ulimi mkono haufutiki.
  • Shika! Shika! na mwenyewe nyuma.
  • Samaki huanza kuoza kichwani.
  • Shibe ya mtu mwingine hanilazi mnene.
  • Saburi ni ufunguo wa faraja.
  • Shoka lisilo mpini halichanji kuni.
  • Shimo la ulimi mkono haufutiki.
  • Sikio la kufa halisikii dawa.
  • Sikio halilali na njaa.
  • Sikio halipwani kichwa/Sikio halipiti kichwa.
  • Sikio halipwani kichwa.
  • Siku njema huonekana asubuhi.
  • Simba mwenda kimya(pole) ndiye mla nyama.
  • Siku utakayokwenda uchi, ndiyo siku utakayokutana na mkweo.
  • Subira ni ufunguo Wa faraja.
  • Subira yavuta heri, huleta kilicho mbali.
  • Sumu ya neno ni neno.
  • Suluhu haija ila kwa ncha ya upanga.
  • Sitafuga ndwele na waganga tele.
  • Simbiko haisimbuki ila kwa msukosuko.

T

  • Tamaa mbele, mauti nyuma.
  • Teke Ia kuku halimwumizi mwanawe
  • Tamu tulikula sote, na uchungu vumilia.
  • Tonga si tuwi
  • Taratibu ndiyo mwendo.
  • Tabia ni ngozi.
  • Tajiri na maliye,maskini na mwanawe.
  • Taratibu ndiyo mwendo.
  • Titi la mama li tamu.

U

  • Udongo uwahi ungali maji
  • Ukenda kwa wenye chongo, vunja lako jicho.
  • Uchungu wa mwana, aujua mzazi.
  • Ucheshi wa mtoto ni anga Ia nyumba.
  • Ukiona neno, usiposema neno, hutapatikana na neno.
  • Ubishi mwingi, huvuta matata
  • Udugu wa nazi hukutania chunguni
  • Ukiona kwako kunaungua kwa mwenzako kunateketea.
  • Uchwelewapo na jua lala pale.
  • Ujinga wa kuuza si baradhuli wa kununua.
  • Ukiona vinaelea, vimeundwa.
  • Ukistaajabu ya Mussa utaona ya Firauni.
  • Ukitaka uzuri sharti udhurike.
  • Ukamba hukatika pabovu.
  • Ukiona neno, usiposema neno, hutapatikana na neno.
  • Ulimi hauna mfupa.
  • Ukikosa titi la mama, hata la mbwa huamwa
  • Ukiona zinduna, ambari iko nyuma.
  • Ukila na kipofu sahani moja, usimguse vyanda.
  • Ukienda kwa wenye chongo, vunja lako jicho.
  • Ukipewa shibiri usichukue pima.
  • Ukupigao ndio ukufunzao.
  • Ukistaajabu ya Mussa utaona ya Fir-Auni.
  • Ukitaja nyoka, shika fimbo mkononi.
  • Ukuukuu wa kamba Si upya wa ukambaa.
  • Ukitaka cha mvunguni, sharti uiname.
  • Ukitaka uzuri sharti udhurike.
  • Ulacho ndicho chako, kilichobaki nicha mchimba lindi.
  • Ulipendalo hupati hupata ujaliwalo.
  • Ulimi unauma kuliko meno.
  • Ulivyoligema utalinywa.
  • Umekuwa bata akili kwa watoto?
  • Umekuwa jeta hubanduki?
  • Umwepuke, mwenda-pweke.
  • Ungalijua alacho nyuki, usingalionja asali.
  • Usiache kunanua kwa kutega.
  • Upikapo samaki, huachi kunuka vumba.
  • Uniponye kwa jua, nitakuponya kwa mvua.
  • Umekuwa nguva, huhimili kishindo?
  • Unamlaumu mwewe, kipanga yuwesha kuku.
  • Ushikwapo shikamana.
  • Usiache mbachao kwa msala upitao.
  • Usigombe na mkwezi, nazi imeliwa na mwezi.
  • Usiyavuke maji usiyoweza kuyaoga.
  • Usitukane wakunga na uzazi ‘ungalipo.
  • Usijifanye kuku mweupe.
  • Usile na kipofu ukamgusa mkono.
  • Usisahau ubaharia kwa sababu ya unahodha.
  • Usisafiriye na nyota ya mwenzio.
  • Usimwamshe aliyelala utalala wewe.
  • Usinivishe kilemba cha ukoka.
  • Usicheze na simba, ukamtia mkono kinywani.
  • Usidharau kiselema chalima kikapita jembe zima.
  • Usipoziba ufa utajenga ukuta.
  • Uta hauui bila upote
  • Uzuri wa mke nguo, wa ng’ombe kulimwa.
  • Uzuri wa mkakasi, ndani kipande cha mti.
  • Uzuri wa godoro wa nje tu, kwa ndani mna pamba
  • Usiwashe taa, nyumbani mwa kipofu.

V

  • Vita havina macho.
  • Vita ya panzi, furaha ya kungu.
  • Vikombe vikikaa pamoja, havina budi kugongana.
  • Vita vya panga, haviamuliwi na fimbo.

W

  • Waraka hauishi maneno.
  • Watafutao, wapata.
  • Wanao usawa gani, hakimu na baradhuli.
  • Wakati wa hari, watu wagombea kisima kimoja.
  • Wapiganapo fahali wawili ziumiazo ni nyasi.
  • Waraka ni nusu ya kuonana.
  • Wema hauozi.
  • Wengi wape.
  • Werevu mwingi, mbele kiza
  • Weka siri moyoni, kunena ni kutolea.
  • Watatuavu, hutatua.
  • Watu wawili hawashibi: mtaka elimu na mtaka ulimwengu.

Y

  • Yu fahali nyati na mali hapati.
  • Yaliyopita, yamepita, yaliyobaki, tuyatupe.
  • Ya kunya, haina wingu.
  • Yapitayo hayabadiliki, na yajayo hayaelimiki.

Z

  • Zito huwa pesi (nyepesi) ukilichukua.
  • Zimwi likujualo halikuli likakwisha.